470;USHAURI: MUONDOE CHUMA ULETE HUYU KWENYE PESA ZAKO.

Mojawapo ya vitu vinavyowafanya watu waishi maisha ya magumu sana hapa duniani ni kukosa namna bora ya kupangilia na kuendesha maisha yao. Kingine ni kwamba wengi wanapenda kuishi maisha ya kuiga, kwasababu umeona jirani yako ana maisha Fulani hivi na wewe unataka uanze kuishi hivyo. Sio vibaya kutamani vitu vizuri kwenye maisha yako lakini ni…

468; Watu Sahihi, Watu Wazuri.

Kwenye Maisha tunawahitaji watu sahihi. Watu Sahihi sio lazima wawe Wazuri kwetu wanaweza kuwa watu wabaya lakini ni sahihi. Kusudi la hao watu kwenye maisha yetu ndio litaamua usahihi wao. Unaweza kukutana na mtu anakuchukia bila sababu halafu kwa kukuchukia kwake kukawa sababu ya wewe kusonga mbele Zaidi. Kuna watu wakikupenda ndio wanakuharibu, badala ya…

467; #usiishienjiani leo: Unajisikiaje Unapofanya kazi Yako?

Ni muhimu sana uweze kujisikiliza na kutambua moyo wako unakwambia nini. Moja ya vitu ambavyo tunakwama ni kushindwa kujisikiliza sisi wenyewe. Unaweza kuwasilikiza wengine lakini huwezi kujisikiliza wewe unataka nini. Mara nyingi ili. Uweze kujua kile unachokifanya kama ni kweli ni kusudi lako ni kuanza kusikiliza unajisikiaje unapofanya. Kama unajisikiaje furaha fulani ambayo haielezeki ndani…

465; #usiishienjiani leo: Kuwa Imara Zaidi.

Chochote unachopitia kwenye maisha yako kama hakijayaondoa maisha yako basi kimekufanya uwe imara zaidi. Tofauti ni kwamba kuna watu badala ya kuwa imara wanakuwa waoga.Umeingia kwenye biashara ukapata hasara pesa zote zikapotea badala ya kuwa imara unakuwa muoga na hujaribu tena. Unaingia kwenye mahusiano unaumizwa halafu inakuwa kama hutaki tena, na unaanza kusema wanaume/wanawake wote…

464; USIISHIENJIANI LEO : Kuwa Glasi Tupu.

Kati ya glasi iliyo tupu na iliyojaa maji siku zote ile tupu ndio hupata nafasi ya kuwekewa maji mengine. Watu wengi tunapenda Kuonekana tunajua kila kitu. Tunapenda Kuonekana sisi kuliko hata vile tunavyovifanya. Ni muhimu ujue kuwa Unapokuwa kama glas tupu maana yake wewe ni mtu unaefanyia kazi yale ujifunzayo. Huachi glasi ikiwa na maji…

Subscribe