HATUA YA 316: Kukosea ni Kujua Njia Nyingi Zaidi.

Ulishawahi kwenda mahali ukapotea njia? Unajua ni faida gani unapata baada ya kupotea njia? Kwanza unakuwa umejua njia nyingine ambayo haiendi kule ulipokuwa unakwenda. Pili utakuwa umegundua njia ambayo itakufikisha kule ulipokuwa unataka kwenda kwasababu ulipopotea uliuliza kisha ukaelekezwa. Sasa kama wewe ulikuwa hujui kule ulipokuwa unakwenda na ukaweza kwenda bila ya kupotea kuna hatari…

HATUA YA 315: Hiki Ndio Kipimo cha Thamani ya Unachokifanya.

Lipo swali moja ambalo unapaswa kujiuliza kila wakati kwenye kile ambacho unakifanya kila siku. Inaweza kuwa ni kazi yako, kipaji, biashara au chochote kile kinachokuhusisha wewe na watu. Ni jambo jema sana kujua maendeleo yako na kama kweli unachokifanya kinaongeza thamani kwa wengine. Lazima ujiulize, Hivi nikiacha leo kufanya hiki kitu Itakuaje? Kama ni ajira;…

HATUA YA 313: Historia Itakuhukumu.

Kuna mambo ambayo tunafanya sasa wakai mwingine tunaweza kuwa tunabishana sana juu ya nani yupo sahihi na nani amekosea. Ukweli unaweza usielewe kwa haraka kwasababu wengi wanaweza kutumia mapenzi binafsi na kuangalia kile wanachokipata kwa wakati huo. Mambo mengine yakiwa magumu katika kuujua ukweli tunaachia muda kadiri muda unavyokwenda ndio tutajua nani alikuwa mkweli na…

HATUA YA 312: Njia Rahisi Zaidi.

Kuna wakati mtu anaweza kuja kuomba ushauri halafu akategemea kwamba utampa njia rahisi Zaidi au shortcut ya kutatua changamoto zake. Wakati mwingine unaweza ukapewa njia ngumu Zaidi lakini yenye manufaa kwako wewe mwenyewe. Kutegemea kupewa njia rahisi ndio kunawafanya wengi waache kufanya vitu sahihi na mwishoe kupotea. Kama utategemea upewe muujiza wa kutatua changamoto yako…