Una nguvu kubwa sana ndani yako. Inawezekana hujawahi kuambiwa hata siku moja. Leo ninakwambia ipo nguvu ndani yako ya kushinda yote ambayo unayapitia sasa. Ipo ngvuvu ndani yako ya kukuwezesha kufikia yale yote unayoyataka. Haijalishi sasa hivi unaona giza. Au unapitia magumu kiasi gani. Tumia uwezo ulio ndani yako kuzishinda changamoto unazopitia sasa. Una nguvu…
JINSI YA KUMALIZA MWAKA KWA USHINDI.
Habari za Leo mwanamafanikio? Siku kuu imekwenda vyema kwangu. Natumaini na kwako pia. Ni siku chache zimebaki katika mwaka lakini tukiweza kuzitumia vyema tutaacha alama ndani ya mwaka huu. Usikubali kabisa kutumia muda huu hovyo Tafuta jambo dogo tu la tofauti ulifanye Zikiwa zimebaki takribani siku nne peke yake tumalize mwaka huu napenda kukwambia…
HATUA YA 13; Ipo Siku.
Hapo zamani kabla ya kutambua ni kitu gani natakiwa kufanya ili nifikie Mafanikio nilizoea kusema ipo siku ndoto yangu itatimia. Ni maneno mazuri sana na ya kutia Moyo lakini kama hakuna unachofanya hiyo ndoto itabakia kuwa ndoto. Ipo siku utatambua haya ninayosema ni Kweli. Huwezi kusubiria mazao wakati hakuna shamba lolote ulilootesha mbegu. Ili neno…
HATUA YA 12; Wewe Rafiki Yangu.
Wewe ni Rafiki Yangu hivyo lazima wakati wote niwe nakwambia Ukweli. Ukweli ni kwamba usipokubali kubadilika mwaka 2017 utakua mgumu zaidi. Wewe Rafiki Yangu usiopoacha kuishi maisha yako halisi utaishia kuteseka moyoni mwako kwa kuwaridhisha wengine. Wewe Rafiki yangu acha kuwa mzembe kila siku nakwambia kusoma vitabu ni muhimu sana lakini unahisi nakutania. Lakini ipo siku…
HATUA YA 11; Furaha yako Inatoka Wapi?
Furaha yako inatoka wapi? Nataka ujiulize leo furaha yako inatokana na nini! Kila mmoja ana jibu lake juu ya chanzo cha furaha yake. Kama furaha yako inaletwa na vitu au watu kuna wakati utakosa furaha. Wakati vitu havipo utakosa furaha, watu wakikuacha utakosa furaha. Kama furaha yako inaletwa na mali nyingi utaishi bila furaha hadi…
HATUA YA 10; Tafuta sababu ya Tatizo
Kila kinachotokea Maishano mwako kinatokea Kwasababu. Changamoto yeyote unayopitia ipo Kwasababu. Ugumu wa Maisha unaopitia upo Kwasababu. Ukosefu wa pesa ulionao upo Kwasababu. Kuachwa na umpendae imetokea Kwasababu. Kudharauliwa kumetokea Kwasababu. Kusemwa kunatokea Kwasababu. Hakuna kinachotokea kwa Bahati mbaya hata siku moja. Kuna sababu nyuma ya lolote linalotokea. Umefanikiwa Kwasababu ulifanya kazi kwa bidii. Badala…
HATUA YA 9; Tabia ya Uvivu.
Tabia ya Uvivu ndio inasababisha wengi wanapata hasara ya maisha pamoja na matatizo mbalimbali. Tabia ya Uvivu mara nyingi huletwa na kuridhika na kile unachokipata. Kama mtu ana uhakika wa kupokea laki nane kwa mwezi anajisahau kabisa kwamba hana umiliki na kazi yake. Badala ya kuongeza bidii na Kutafuta chanzo kingine cha mapato mtu huyu…
HATUA YA 8; UADILIFU
Uadilifu ni kitu cha muhimu sana kwenye Maisha yetu ili kutuwezesha kujenga historia nzuri. Watu wengi wanakosa uadilifu ndio maana biashara zao zinakufa baada ya muda mfupi. Uadilifu ni sifa ambayo itakufungulia milango mingi ya fursa huko mbeleni. Kama utakosa uadilifu katika hatua hizi za mwanzo unaanza kuonyesha picha ya wewe ulivyo na huko mbeleni…