Offa, Ya Vitabu Bora Mwezi April. https://jacobmushi.co.tz/offa-offa-offa-ya-vitabu-bora-mwezi-april/ “Because a thing seems difficult for you, do not think it impossible for anyone to accomplish.” ― Marcus Aurelius Kwasababu kitu kimeonekana ni kigumu kwako, usifikiri haiwezekani kufakiwa kwa wengine pia. Kuna tabia ya wengi kupenda kutoa mfano wa walio shindwa jambo ambalo wameona unataka kufanya. Pia mtu mwingine…
#HEKIMA YA LEO: Unamwangalia Nani?
Kila mmoja wetu kutokana na anachokifanya kuna mtu aliefanikiwa zaidi yake. Ni muhimu sana kujua unaemtazama na ni vitu gani unajifunza kwake. Hakuna mtu ambaye atakuwa anaenda tu bila kuwa na mtu anaemwangalia. Unapaswa kujifunza sana ujue ni mbinu gani wanatumia hadi wanapata matokeo makubwa. Usikubali kubaki kama mtu asiye na mwelekeo wa maisha. Wapo…
#HEKIMA YA LEO: Unyenyekevu Utakulinda.
Unawafahamu watu ambao wakiwa na shida wanakuja kwako kwa upole wakinyenyekea sana. Lakini wakishapata wanasahau na kuanza kuonyesha tabia zao halisi. Wako watu wa aina hii wengi kwenye jamii yetu. Wakiwa chini wanakuwa wanyenyekevu na wapole sana. Wakipata fedha au cheo utaanza kujua tabia zao za kweli. Rafiki yangu nakuomba usiwe mmoja watu wa aina…
Offa Offa Offa, Ya Vitabu Bora Mwezi April.
Offa Hii Imekwisha muda wake. Unaweza kupata vitabu kwa bei za kawaida hapa.. https://jacobmushi.co.tz/patavitabu/
HATUA YA 317: Umejifunza Nini?
Inawezekana wewe ni Mkristo na umekuwa unaikumbuka hii siku kuu ya Pasaka kila mwaka, lakini lipo swali la muhimu kujiuliza. Je tunajifunza nini? Pia haijalishi wewe ni dini nyingine yeyote au pia huamini kama kuna Mungu, bado unapaswa kuangalia katika namna ya kujifunza. Lipo jambo moja kubwa ambalo kila mmoja wetu anaweza kulipata kwenye siku…
#HEKIMA YA LEO: Wakati Mwingine Jifunze Kuyatazama Mambo Jinsi Yalivyo Kwanza…
Ni vyema kuelewa kwamba kuna tofauti ya kuwa chanya kwenye mambo na kupotezea ukweli halisi wa jambo lenyewe. Kuna nyakati ili uweze kutatua mambo kwenye maisha yako inakupasa uanze kuyaelewa hayo mambo yakoje. Mfano una matatizo kwenye familia yako hata ukiwa chanya kivipi, na ukaweza kuyaona hayo matatizo sio kitu hakubadilishi ukweli kwamba hayo ni…
HATUA YA 316: Kukosea ni Kujua Njia Nyingi Zaidi.
Ulishawahi kwenda mahali ukapotea njia? Unajua ni faida gani unapata baada ya kupotea njia? Kwanza unakuwa umejua njia nyingine ambayo haiendi kule ulipokuwa unakwenda. Pili utakuwa umegundua njia ambayo itakufikisha kule ulipokuwa unataka kwenda kwasababu ulipopotea uliuliza kisha ukaelekezwa. Sasa kama wewe ulikuwa hujui kule ulipokuwa unakwenda na ukaweza kwenda bila ya kupotea kuna hatari…
HATUA YA 315: Hiki Ndio Kipimo cha Thamani ya Unachokifanya.
Lipo swali moja ambalo unapaswa kujiuliza kila wakati kwenye kile ambacho unakifanya kila siku. Inaweza kuwa ni kazi yako, kipaji, biashara au chochote kile kinachokuhusisha wewe na watu. Ni jambo jema sana kujua maendeleo yako na kama kweli unachokifanya kinaongeza thamani kwa wengine. Lazima ujiulize, Hivi nikiacha leo kufanya hiki kitu Itakuaje? Kama ni ajira;…