MAHALI SAHIHI PA KUPATA MSAADA WAKATI WA SHIDA AU TATIZO. Na Steven Mshiu I. Kipindi fulani niliazimia kufanya kufanya biashara fulani, na kwa kuwa ilikuwa ni biashara nikaamua kumshirikisha mmoja wa aliyekuwa rafiki yangu katika lile eneo nililokuwepo. Baada ya kumshirikisha tu, akaniambia nyie ndio wachaga mliotumwa pesa mjini. Kwa kweli utatoboa tu. Nilifurahia kwa…
All posts in USIISHIE NJIANI
Faida 5 za Kusoma Vitabu.
Ili uweze kuwa na mwili wenye afya bora lazima ule vyakula bora na kufanya mazoezi. Vilevile kwenye akili yako ni vyema ukapata maarifa ambayo yanakufanya uwe na ufahamu bora. Watu wenye uwezo sana ukiacha wale ambao wana uwezo wa kipekee toka wanazaliwa wengi wanaongeza uwezo wao kwa kusoma vitabu. Soma Kitabu: SIRI 7 ZA KUWA…
#HEKIMA YA LEO: Jambo Hili Lisikukoseshe Raha.
Kuna mambo ambayo yanaweza kukutesa na kukusumbua sana kwenye maisha yako. Kuna mengine yanakuwa mzigo mzito sana ndani yako. Kuna mahali unafika unajisikia kuchoka kabisa na unakuwa umekata tamaa kabisa. Kutokana na ugumu wa mambo mengine wengine hufikia maamuzi ya kutaka kujiua. Neno langu kwako leo ni kwamba usichoke, kuna mambo hata pesa haiwezi kuwa…
#HEKIMA YA LEO: Tofauti Kukosolewa kwa Uzuri na Kukatishwa Tamaa.
Ushawahi kuona mtu amefanya jambo kwa kujiamini sana sasa katika kujiamini kwake kupita kiasi akajikuta haoni hata makossa yake. Inapotokea watu ambao wanamtazama wakamwambia kwamba hapo unakosea, usifanye hivyo fanya hivi. Yeye anaanza kuchukia na kuona kwamba ameonewa, au wale watu wanaomwelekeza wanamwonea wivu. Ukitaka kusonga mbele na kukua Rafiki yangu lazima uweze kutofautisha kati…
Sababu kumi za kwanini unahitaji watu ili kufanikiwa maishani
Umeshawahi kuangalia mashindano yoyote? Au sherehe za ugawaji wa tunzo?/ Bai kama umewahi kuangalia kuna kitu ambacho kinajirudia kwa watu wote wanaoshinda. Huwa wanatoa insha ndefu na kutaja majina ya watu waliowasaidia kufika hapo walipo, na wakati mwingine huwa wakilia kwa furaha ya jinsi hao watu walivyohusika katika ushindi wao wa hiyo tunzo au hayo…
#HEKIMA YA LEO: Kubali Kupitia Maumivu, Na Mchanganyiko.
Unajua mboga tamu ilipitia maumivu kwenye moto mkali jikoni. Ni rahisi sana kusifia utamu wa mboga bila ya kujua ni gharama gani imelipwa wakati wa kuitengeneza. Ili mboga iwe tamu lazima kuwa na mchanganyiko wa viungo ambavyo vitaleta ladha ya tofauti. Ladha ya mboga inatokana na mchanganyiko wa viungo. Kwenye Maisha ili uweze kuwa wa…