1 Wafalme 17:4,6 [4] Itakuwa utakunywa maji ya kile kijito; nami nimewaamuru kunguru wakulishe huko. 6. Kunguru wakamletea mkate na nyama asubuhi, na mkate na nyama jioni, akanywa maji ya kile kijito. Nimewatafakari wale Kunguru waliomlisha Elia nyama na mkate tena kipindi ambacho nchi ilikuwa imekosa mvua karibu miaka mitatu (maana yake kulikuwa na njaa)…
All posts in AFYA, HEKIMA NA UTAJIRI
507; Yanapotokea Usiyoyatarajia.
Ni kweli mtu unaweza kuwa na fikra hasi juu ya Maisha yako lakini hakuna mtu hata mmoja anaetaka zile fikra hasi zitokee. Kinachomfanya mtu ajikute anawaza sana ni kwasababu ya hofu. Kila mtu huogopa pale anapowaza mambo mabaya yatatokea siku moja, kila mmoja anaweza kusita kuchukua hatua pale anapohisi kuna jambo baya litatokea kwenye kile…
506; Nilimwona Akiingia Gesti Jana Jioni
Ni mara ngapi umewahi kuambiwa kuhusu wengine, mfano; “Nilimwona Fulani akiingia Gesti Jana”, “Fulani ana Mwanamke Mpya” na mengine mengi. Ukweli ni kwamba huenda umeyasikia sana kutoka kwa watu au hata wewe ulishawahi kumwambia mtu. Sasa nikwambie kitu kimoja, hayo ni maoni tu ya watu ambayo hayana ukweli halisia. Ngoja nikupe kisa hiki, Miaka michache…
505; Mama Usimtukane Mwanao.
Nilikuwa napita katika mitaa ya uswahilini hapa Tandika, sasa nikakutana na mama mmoja anamwogesha mwanae wa kiume. Sasa yule mtoto akawa anasumbua sumbua, yule mama akamporomoshea matusi mazito ya nguoni. Yaani alimuita viungo vyake yeye mwenyewe vya siri, nilisikitika sana, nikawaza huyu mtoto akija kupata akili sawasawa akaja kujua maana ya kile anachotukanwa na mama…
504; Nyama Kilo 1 ni Tsh elfu moja.
Embu jiulize leo bei ya nyama kilo moja ni Tsh elfu tano hadi elfu saba kulingana na maeneo, sasa ukipita mahali ukakuta kuna nyama ya ng’ombe safi kabisa imenona wanauza kilo moja shilingi elfu moja utavutiwa kwenda kununua? Jibu rahisi sana na ambalo kila mmoja atafanya ni HAPANA. Na itakuwa hapana kwasababu haiwezekani nyama iuzwe…
503; Msikilize Mungu.
Wanadamu wana tabia ya kuongea bila kufahamu na ukifanya makossa ukawasikiliza wanaweza kukupoteza. Tukimtazama kijana Daudi aliekuwa mchunga kondoo porini, baba yake na ndugu zake walimchukulia kama mchunga kondoo, na kijana mdogo tu. Lakini Mungu mwenyewe alikuwa ameshamchagua kuwa mfalme wa Israel. Kwa akili za kibinadamu mara zote tunatazama nje. Watu wakikutazama kwa nje wanaona…