Tunaishi kwenye dunia ya watu wenye tabia za aina tofauti tofauti. Wengine wenye kukera, kuudhi, kukasirisha na kila aina ya ubaya. Wengine ni wapole wanaweza kusikiliza watu vizuri na hata kama utawaudhi kamwe hawataweza kukasirika na wewe. Sasa tukiachana na hao watu ambao tunaweza kuwazungumzia juu ya tabia zao inatakiwa wewe binafsi uanze kujifikiria wewe…
All posts in MBINU ZA MAFANIKIO
MAMBO 4 AMBAYO NI LAZIMA UKUTANE NAYO NJIANI KATIKA KUTIMIZA NDOTO YAKO.
Katika safari ya mafanikio unapoamua kujikana na kusema ni lazima ndoto yako itimie kuna mambo mengi utapitia kwenye Maisha. Zipo aina ya changamoto ambazo hujirudia kama tu ndoto zako ni kubwa na umeamua kufika mbali. Kama umeamua kuwa tofauti na wengine kuna mambo ambayo ni lazima yakutokee tu haijalishi hao watu ni aina gani. Ni…
Mafanikio Ni Kila Siku.
Maamuzi chanya madogo madogo unayofanya kila siku ndio yataamua aina ya Maisha utakayokuja kuishi miaka 5/10/20 ijayo. Fanya maamuzi sahihi, chukua hatua bila kukata tamaa. Mafanikio sio hatua kubwa Fulani ambayo unatakiwa uifikie ndio tuseme umefanikiwa bali ni matokeo chanya kidogo kidogo ambayo unayapata kila siku kwa hatua unazochukua. Kama kila siku kuna jambo unakuwa…
UNATAKA ULINZI? JUA KITU HIKI CHA MUHIMU KWENYE MAISHA YAKO.
Mwaka 2004 ulikuwa ni mwaka ambao ungeweza kuwa sababu ya wewe kutokusoma hiki ninachokiandika leo wala kufahamu kama niliwahi kuwepo kwenye ramani ya dunia hii. Lakini kwasababu ya kusudi la Mungu ambalo aliweka ndani yangu akaweza kunipa kibali nikapata tena nguvu ya kuendelea kuishi na sasa unaweza kunisikia na kusoma Makala ninazoandika. “Ilikua ni jioni…
Jifunze Kwa Mtoto
Kuna nyakati kwenye maisha tunapitia hali ambazo zinatulazimisha kufanya mambo tusiyohitaji ila ni kwasababu tunaisikiliza mili yetu. Sio kila hali ambayo unaisikia kwenye mwili wako inahitaji kufanyiwa kazi. Ukiwa na mtoto mdogo utaweza kuniambia kwamba sio kila anacholilia mtoto unampatia. Mfano anatakiwa kulala na yeye anataka kwenda kucheza huwezi tu kumruhusu kwasababu ametaka. Anatakiwa kula chakula akalilia…
JINSI YA KUJIJENGEA TABIA YA KUWA MSOMAJI WA VITABU KILA SIKU.
Habari za leo Rafiki yangu na msomaji wa mtandao wa USIISHIE NJIANI? Ni matumaini yangu kuwa bado hujaishia njiani kwenye safari yako ya mafanikio. Kila siku kuna hatua unapiga kutokana na yale unayojifunza hapa kila siku. Leo tunakwenda kuona ni jinsi gani ya kujijengea tabia ya kujisomea vitabu kila siku. Mojawapo ya changamoto kubwa inayowakumba…