HATUA YA 195: Kizazi cha Kuona Kwanza na Kuamini.

Tupo kwenye kipindi ambacho watu wake hwaamini tena mpaka waone. Kizazi ambacho hakiamini matendo ya Imani mpaka kione kwa macho ya damu na nyama. Tuna watu wengi sana ambao hawawezi kuamini chochote unachowaambia bila ya kuona ishara ya papo kwa papo. Kama huwezi kujenga Imani kwanza ndipo uone matokeo utaishia kudanganywa kwenye mambo mengi ya…

HATUA YA 194: USIKUBALI PESA IKUTAWALE.

Mojawapo ya dalili za kuanguka kimafanikio ni pale pesa inapoanza kumtawala mtu. Tunaposema mtu ametawaliwa na pesa ni pale pesa inapofanya maamuzi badala ya mwenye pesa kufanya maamuzi. Ukiona umefikia kiwango ambacho ukipata pesa kila mtu anajua una pesa na zikiisha kila mtu anajua zimeisha ujue wewe pesa imekutawala.   Ukiona umefikia mahali pesa ndio…

HATUA YA 193: Ukitaka Kuaminika…

Ukitaka kuaminika usiwe mtu wa kubadilika badilika kutokana na mazingira uliyopo au unapokuwa na watu wa aina Fulani. Ukitaka kuaminika kuwa wewe siku zote. Ukitaka kuaminika kuwa mtu ambaye unatabirika yaani watu wakikuacha mahali wanaamini hutabadili tabia. Unayafahamu maji? Maji ukiyaweka kwenye ndoo yatakaa na yatabeba umbo la ndoo. Vilevile maji ukiyaweka kwenye mfuko yatakaa…

HATUA YA 192: Vitu 2 Unavyotakiwa Kuvijua Ili Uwe na mwelekeo wa Maisha Bora.

Kitu ambacho kila mmoja anakipigania ni Maisha bora.  Na maisha bora ni pale unapopata kile unachokitaka pamoja na kufurahia Maisha yako kwa ujumla na kile unachokifanya. Tukiweza kuujenga msingi bora wa Maisha yetu hatuwezi hata siku moja kujutia aina ya Maisha tunayoishi. Zipo sehemu mbili za muhimu sana kama utaweza kujenga msingi wako hapo Maisha yako…

HATUA YA 191: Usiishi Maisha ya Dharura.

Kuna dharura zinajitokeza wakati upo kwenye shughuli zako na kuna dharura zinatokea na wewe upo upo tu hujui cha kufanya. Kama utashindwa kutofautisha vitu vya dharura na vitu vya muhimu kwenye Maisha yako utajikuta unapoteza mwelekeo wa Maisha yako. Vitu vya dharura ni vitu vile ambavyo mara nyingi vinajitokeza kwenye ratiba yako na hukuwa umevipangilia.…

HATUA YA 189: Mbinu 3 za Kuweza Kuwa Wiki Bora.

Maisha yako yapo mikononi mwako, ukishindwa kupangilia siku yako vizuri unapanga kuipoteza. Ili uweze kuwa na juma lenye uzalishaji bora ni vyema ukawa na ratiba yako ya kila wiki. Jua ni vitu gani vya muhimu ambavyo utakwenda kuvifanya kabla wiki haijaanza. Pangilia Wiki Yako Kabla Hujaianza. Kwa kawaida wote siku ya Jumapili tunaitumia kama mwisho…