HATUA YA 201: Ukitaka Kutumia Zaidi..

Kanuni ya Umaskini ni kutumia Zaidi ya unachozalisha. Kama unataka kubakia kuwa maskini endelea kuwa na matumizi makubwa kupita uwezo wako wa kuzalisha. Kama wewe ni mkulima ukizoea kula Zaidi ya unachozalisha mwisho wa siku utakula na mbegu inayokuzalishia. Kama wewe ni mfanyabiashara ukizoea kutumia Zaidi ya unachopata utaanza kula mtaji. Kanuni ya mafanikio inasema…

HATUA YA 199: Wasikilize Lakini Amua Wewe.

Kwenye vitu tunavyovifanya kila siku tunakutana na maoni ya wengine kila siku. Jambo la muhimu ni kwamba usikatae kupokea maoni ya watu. Kitu unachotakiwa ni kuyachuja na kuchagua yale ambayo unaona yanafaa kule unapoelekea. Usiruhusu watu wakufanyie maamuzi maana wewe ndie unajua unapoelekea. Usiwape wengine madaraka ya kuamua wewe uwe na baadae ya aina gani.…

HATUA YA 196: Kuna Mahali Ulisababisha.

Mambo mabaya yote yanayotokea kwenye Maisha yako sio kwa bahati mbaya kuna mahali uliyasababisha yakatokea. Badala ya wewe kuchukua muda mwingi kulaumu na kulalamika jiangalie kwa upande wako unahusikaje kusababisha. Tuchukue mfano rahisi watu wawili wanagombana hadi kutaka kupigana, ukikaa na mmoja wapo ukamuuliza ilikuaje ataanza kumtupia lawama mwenzake. Lakini ukweli hadi wakafikia kugombana yeye…