HATUA YA 387: Ukikosea Utapigwa..

Shule ya Sekondari niliyosoma kulikuwa na waalimu ambao nawakumbuka mpaka sasa. Mwalimu mmoja alisifika sana kwa kufundisha vizuri sana, Mwalimu mwingine alisifika sana kwa kuchapa viboko. Wote ni waalimu lakini mmoja ana sifa ya kazi yake na mwingine ana sifa ya kuchapa. Hapa kuna kitu cha kujifunza Rafiki wewe unataka sifa gani kwenye kile unachokifanya?…

HATUA 386:  Ndoto Yako Inakuhamasisha?

Mhamasishaji wa Kimataifa Les Brown aliwahi kusema kwamba sio kuwa wtau hawana malengo watu wana malengo lakini ni madogo sana kiasi kwamba wanayatimiza haraka sana bila ya changamoto yeyote. Unapaswa kuweka malengo makubwa ambayo hata usipoyafikia basi yatakuwa yamekuwezesha ufike mbali sana. Ndoto yako inatakiwa iwe kubwa kiasi kwamba inakuhamasisha kuamka asubuhi na mapema uende…

HATUA YA 385: Ukitaka Kueleweka Acha Kutafuta Kueleweka.

Ukweli ni kwamba ukitafuta kueleweka utakuwa unawachanganya watu badala ya watu kukuelewa. Kitu ambacho unaweza kukifanya pekee ni kuendelea kufanya kile unachoamini, endelea kuwa wewe hata kama watu wanakupinga. Kutaka kueleweka na kila mtu ni kazi ngumu sana ambayo wengi walishashindwa. Ukianza kuishi kile unachokiamini kuna watu wengi wataendelea kukufuata kwasababu wataanza kuamini kile unachokifanya.…

Subscribe