Katika vitu ambavyo hatuwezi kuvibadili katika maisha yetu ni historia huwezi kubadili tena vile vitu ulivyowahi kuvifanya jana, juzi na miaka iliyopita. Kitu cha muhimu ni wewe kuweza kugundua kwamba ulikosea wapi na uanze kutumia wakati huu ulionao sasa kufanya yaliyo sahihi. Hata uwe umefanya mabaya kiasi gani huwezi kuyafuta huwezi kubadili chochote unatakiwa utambua…
Ni nini kitasababisha watu walie siku ya kufa kwako?
Watu wengi huchukulia maisha ni kitu cha kawaida sana mpaka wanaamua kuishi kula, kuzaa na kusubiria siku ya kufa basi. Ukweli ni kwamba kama ulikua unawaza hivyo umeshapotea na kama umeweza kusoma hapa leo basi ni wakati wako wa kutafuta njia sahihi, ni wakati wako wa kujitafuta wewe mwenyewe. Kama kuna kazi ambayo ni ngumu…
Ni nini kinakufanya wewe ufanye kazi kwa bidii?
Katika maisha yetu kila siku tuna watu wanaofanya kazi kwa bidii sana kila siku kwenye ajira zao, kwenye biiashara zao, kwenye vipaji vyao na kadhalika. Kitu kinanachowatofautisha watu hawa mara nyingi ni matokeo ya kile wanachokifanya. Kila mmoja atapata kutokana na alichokitoa. Mara nyingi nikikutana na watu wengi hua napenda kuwauliza swali hili, “Ni kitu…
MAMBO YA MUHIMU KUTAZAMA ILI TUWEZE KUONA MWANGAZA WA MAFANIKIO KILA WAKATI
Tangaza msamaha Tangaza msamaha kwa waliokutendea mabaya yeyote kwenye maisha yako.Ulitelekezwa ukiwa mtoto mdogo tangaza msamaha leo. Uliumizwa na mpenzi wako uliempenda sana hata ukasema hutakaa umsamehe tangaza msamaha leo. Ulidhulumiwa chochote na mtu mtangazie msamaha leo. Ulifukuzwa kazini kwa hila watangazie msamaha leo. Hakikisha huna kinyongo chochote na mtu moyoni mwako. Nakuhakikishia mambo yako…
Vitu 7 vya muhimu kufahamu ili uweze kusonga mbele.
Kuna vitu saba vya muhimu ambavyo ni lazima uvijue ili uweze kuanza kusonga mbele kimaisha. Ukiweza kuvichukua na kuingiza kwenye maisha yako utaona matokeo yake. 1.ELIMUKitu cha kwanza kwenye vitu FISA ni Elimu. Tunapozungumzia elimu hatumaanisha uwe na elimu ya chuo kikuu au ujue kila kitu hapa unatakiwa uwe na ufahamu wa kutosha juu ya…
Fanya tena
Matokeo ya kile unachokifanya yanaweza yasitokee kama ulivyotarajia au kupanga haimaanishi kwamba unachokifanya sio sahihi. Kuna kua na sababu nyingi za kile ulichofanya kinapokuja na matokeo tofauti. Inawezekana wewe ndie mwenye tatizo. Kabla hujaamua kuacha kufanya au kutafuta njia nyingine kaa chini utafakari ili ufahamu chanzo halisi cha tatizo. Watu wengi hukata tamaa haraka sana…
Unawezaje kubadili hali uliyonayo sasa hivi?
Kabla hujaanza kubadili chochote lazima ufahamu chanzo cha hali uliyonayo kimesababishwa na nini. Ukweli ni kwamba mfumo wako wa maisha unajengwa na mambo haya yafuatayo. FIKRAKila kitu kinaanzia kwenye mawazo/fikra zetu kama unajiona upo kwenye hali mbaya sana kipindi ujue imesababishwa na mawazo uliyoyawaza kipindi Fulani. Kama kuna kitu cha muhimu cha kuchunga ni mawazo…
Fanya maamuzi.
Tatizo kubwa tulilonalo hapa nchini sio pesa. Tatizo kubwa tuna watu wengi ambao ni waoga kufanya maamuzi. Mtu anakutana na fursa nyingi anahamasika Lakini tatizo lipo kwenye kuchukua hatua. Upo hivyo ulivyo leo kwa sababu ya maamuzi uliyoyafanya siku za nyuma pia vile vile upo vile ulivyo haujaendelea, kwa sababu ya woga uliogopa Kufanya maamuzi…