Tabia ya Kutoa inavyohusika katika mafanikio yako.

Habari za leo rafiki yangu. Naamini unaendelea vyema na maisha yako. Ni siku nyingine tena ambayo tunajifunza tabia mbalimbali zinahusika katika kukuvuta kwenye mafanikio makubwa. Leo tunakwenda kutazama tabia ya Kutoa na Kupokea katika maisha yetu. Kutoa, ni kitendo cha kupeleka vitu ulivyonavyo kwa jamii inayokuzunguka. Iwe umetoa kitu kama msaada au umetoa kitu ili…

Jinsi Tabia ya Shukrani inavyoweza kukupeleka kwenye mafanikio makubwa.

Habari za leo ndugu msomaji. Ni matumani yangu kwamba unaendelea vyema na mapambano katika kuifikia ndoto yako. Ni kweli kabisa unaweza kuifikia ndoto yako na mimi kazi yangu ni kukupa njia na vitu vya muhimu vya kufanya ili ukifika kule unakoenda udumu. Leo tunaingalia tabia ya Shukrani ambavyo inaweza kutumika katika kumwezesha mtu afikie mafanikio…

Jinsi Tabia ya Uaminifu inavyoweza kukuletea Fursa.

Habari za leo ndugu yangu. Natumaini unaendelea vyema katika mapambano. Leo nataka tukajifunze tabia ya Uaminifu ambayo inaweza kukusababishia wewe uendelee kupata fursa nyingi kila siku. Uaminifu ni nini? Kwa lugha ya kiingereza tunaweza ni maneno loyalty, fidelity kutekeleza wajibu wako na kile ulichokiahidi kwa usahihi inawezekana ni kwa rafiki yako, mpenzi wako, mke, kazini,…

TUMIA UWEZO WAKO WA KUVUMBUA VITU

“Wote tumezaliwa duniani ili kuifanya dunia kua bora. Kuitoa pale tulipoikuta na kuipeleke sehemu nyingine nzuri Zaidi.” Kila binadamu ana uwezo wa kipekee sana ndani yake na ana nguvu kubwa sana ndani yake vyote hivi tumezaliwa navyo. Tumeanza kuvigundua kidogo kidogo kadiri tunavyojifunza kila siku. Tumezaliwa na zawadi nyingi sana ndani yetu ambazo tunatakiwa tuziache…

UNA ZAWADI NDANI YAKO.

Kila mmoja ana kitu cha kipekee sana ndani yake ambacho amezaliwa nacho. Ni muhimu sana kutambua zawadi uliyozaliwa nayo ili uweze kuitumia kuyafanya maisha ya wengine kua mazuri. Kupitia unachokifanya kuna mtu anaguswa sehemu. Kwa kupitia unachokifanya kuna maisha ya mtu yanabadilika. Haijalishi ni kidogo kiasi gani lakini kuna mtu anafurahia kazi yako. Jiangalie hapo…